IMANI MAPENZI NA NGONO NDIYO VITU VYENYE NGUVU KULIKO MIHEMKO MINGINE YOTE MIKUBWA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

IMANI MAPENZI NA NGONO NDIYO VITU VYENYE NGUVU KULIKO MIHEMKO MINGINE YOTE MIKUBWA



SURA YA 3
IMANI:
Kuona na Kuamini Katika kufikia Shauku
(Hatua ya pili Kuelekea utajiri)

Imani ndiyo mkemia mkuu wa akili. Imani inapochanganywa na msisimko(mtetemo) wa fikra, akili ya ndani mara moja huuchukua msisimko, na kuutafsiri kuwa katika kipimo cha imani na kuusafirisha kwenda kwa nguvu kuu isiyokuwa ya kawaida sawa kama ilivyo kwenye suala la sala.

Imani, mapenzi(upendo) na ngono(kujamiiana) ndiyo vitu vyenye nguvu zaidi kushinda mihemko yote mikubwa. Vitu hivi vitatu vinapochanganywa, vina athari ya ‘kugeuza’ mtetemeko wa fikra kuwa katika namna ambayo huweza kufika mara moja kwenye akili ya ndani ambapo hugeuzwa kuwa katika mfumo wa kiimani(kiroho), mfumo ambao ndiyo pekee wenye uwezo wa kuwasiliana na Nguvu kuu(Mungu).

Mapenzi(upendo) na Imani ni vitu vya kiakili(nafsi), huhusika na upande wetu wa kiroho. Ngono(kujamiiana) ni tendo la kibaiolojia zaidi, na huhusiana tu na vitu vya nje vinavyoonekana. Mchanganyiko wa mihemko hii mitatu una athari za kufungua moja kwa moja mstari wa mawasiliano baina ya akili ya kawaida ya kufikiria na ule uwezo usiokuwa wa kawaida(Nguvu kuu)

Jinsi ya Kujenga Imani.
Imani ni hali ya akili ambayo inaweza ikaambukizwa au kutengenezwa kupitia kukiri au maelekezo yanayojirudia kwenye akili ya ndani kwa kupitia kanuni za kujishauri binafsi. Kama kielelezo angalia nia yako kwa mfano ya kukisoma kitabu hiki. Kimsingi lengo ni kupata uwezo wa kugeuza mawimbi ya fikra yasiyoshikika ya shauku kuwa kitu(mwenzake) kinachoshikika kama Pesa.

Kwa kufuata maelekezo yaliyoorodheshwa kwenye sura ya 3 juu ya Kujishauri na Sura ya 11 juu ya Akili ya ndani, unaweza ukaishawishi akili ya ndani kwamba unaamini utapokea kile ulichokiomba. Itaifanyia kazi imani hiyo na kuirudisha tena kwako katika mfumo wa imani, ikifuatiwa na mipango kamili ya kulifikia lengo lako.

Njia ambayo mtu huitumia kujenga Imani, ambapo haikuwepo hapo kabla ni ngumu sana kuielezea. Kwa kweli ni ngumu karibu sawa na ambavyo huwa ngumu kumuelezea kipofu jinsi rangi nyekundu ilivyo. Imani ni hali ya akili ambayo unaweza ukaijenga kwa hiyari yako mwenyewe baada ya kuwa umeshazifahamu vilivyo hatua 13 kuelekea utajiri ndani ya hiki kitabu.

Kurudiarudia kuiambia kwa dhati akili yako ya ndani ndiyo njia pekee inayojulikana ya kujenga hisia kubwa za imani kwa hiyari. Pengine maana yake inaweza ikawa wazi zaidi kupitia maelezo yafuatayo ya namna watu wakati mwingine wanavyogeuka kuwa wahalifu.

Yalielezwa katika maneno ya mtaalamu mashuhuri wa mambo ya uhalifu kwamba; “Mara ya kwamza watu wanapokuwa karibu na maswala ya uhalifu huwa wanachukizwa nao, Ikiwa wataendelea kwa muda kuwa nao karibu, huuzowea na kuuvumilia. Ikiwa wataendelea kuushuhudia kwa kipindi kirefu zaidi, mwishowe huukumbatia kwa moyo na kushawishika nao.”

Hii ni sawa na kusema kwamba, msukumo wowote wa fikra unapopitishwa kwenye akili ya ndani mara kwa mara, mwisho wake hukubalika na kufanyiwa kazi. Akili ya ndani huendelea kutafsiri msukumo huo kwenda kwenye kitu kinachoshikika chenye ukubwa sawa na msukumo huo kupitia njia za kivitendo zaidi zilizokuwepo.

Sambamba na hilo zingatia tena kauli hii, MAWAZO YOTE YALIYOPEWA HISIA KALI NA KUCHANGANYWA NA IMANI, huanza mara moja kujitafsiri yenyewe kuwa kitu halisi kinachoshikika na kinacholingana nayo.

Mihemko au “hisia” sehemu ya fikra, ni vigezo vinavyoyapa mawazo(fikra)  uhai, maisha na vitendo. Mihemko ya imani, mapenzi na ngono, inapochanganywa na msukumo mwingine wowote ule wa fikra, huipa uwezo mkubwa zaidi kushinda vile ambavyo mhemko mmoja mmoja ungeweza kuwa ukiwa peke yake. Siyo tu misukumo ya fikra iliyochanganywa na Imani, lakini pia ile ambayo iliyochanganywa na mihemko chanya yeyote ile au mihemko hasi yeyote ile- inaweza ikaifikia na kuiathiri akili ya ndani.

Kutokana na kauli hii, utatambua kuwa akili ya ndani itatafsiri msukumo wa fikra wenye asili hasi au ya kubomoa kwenda katika kitu kinachoshikika, sawasawa kama vile itakavyotenda kwa msukumo wa fikra wenye asili chanya au ya kujenga. Hii ndiyo sababu ya hali isiyokuwa ya kawaida, ya mamilioni ya watu kukumbwa na kile kinachotajwa kama, “Bahati mbaya” au “Mkosi”

Mamilioni ya watu huamini wenyewe “kuangamizwa” kwenye umasikini na maanguko, kutokana na nguvu za ajabu ambazo huamini hawawezi kuzidhibiti. Wao ndio waumbaji wa “Mikosi” yao wenyewe kutokana na hii imani hasi, ambayo huchukuliwa na akili ya ndani na kutafsiriwa kuwa katika kitu halisi kinacholingana nayo.

Hapa ni mahali muafaka pa kupendekeza tena kwamba, unaweza ukanufaika kwa kuingiza katika akili yako ya ndani Shauku yeyote ambayo unatamani kuitafsiri kuwa katika kitu halisi, au kiasi cha fedha, katika hali ya matamanio au imani kwamba badiliko kweli linatokea.

Imani yako au Itikadi ni kiungo kinachoamua kitendo cha akili yako ya ndani. Hamna kitu kitakachokuzuia “kuidanganya” akili yako ya ndani wakati unapoipa maelekezo kupitia, kujishauri binafsi, kama nilivyoidanganya akili ya ndani ya kijana wangu. Kuufanya “uwongo” kuwa kweli zaidi, jifanye mwenyewe tu kama vile ambavyo ungekuwa ikiwa UNGELIKUWA TAYARI UNAMILIKI KITU UNACHOKITAKA unapokuwa ukiwasiliana na akili yako ya ndani. Akili ya ndani itageuza kuwa kitu halisi kinacholingana, kwa kutumia njia za moja kwa moja  zaidi na za kivitendo zilizokuwepo, maelekezo yeyote itakayopewa yakiwa katika hali ya imani au itikadi ni kwamba yatatekelezwa.

Ukweli mengi yameelezwa kutoa mahali pa kuanzia ambapo mtu anaweza, kwa kupitia mazoezi na vitendo, kupata uwezo wa kuchanganya imani pamoja na maelekezo mengine yeyote yanayotolewa kwa akili ya ndani. Ukamilifu utakuja kwa kupitia kufanya mazoezi ya vitendo. Hauwezi ukaja tu hivihivi kwa njia ya kusoma maelekezo.

Ikiwa ni kweli kuwa mtu anaweza akawa mhalifu kwa kuishi miongoni mwa uhalifu (na huu ni ukweli unaofahamika), ni ukweli sawa na huo kwamba mtu anaweza akaikuza imani kwa kuishauri kwa hiyari akili yake ya ndani kwamba anayo imani. Akili huja mwishowe, kuendana sawa sawa na asili ya ushawishi ambao umekuwa ukitawala. Tambua ukweli huu na utaelewa ni kwanini ni muhimu kwako kuchochea mihemko chanya kama nguvu zinazotawala katika akili yako, na kuivunjamoyo – na kuiondoa - mihemko hasi.


Akili iliyotawaliwa na mihemko chanya  huwa makao mazuri kwa hali ya akili ijulikanayo kama  Imani. Akili iliyotawaliwa kiasi hicho inaweza kwa hiyari yake, kuipa akili ya ndani maelekezo ambayo itayakubali na kuyafanyia kazi mara moja.


0 Response to "IMANI MAPENZI NA NGONO NDIYO VITU VYENYE NGUVU KULIKO MIHEMKO MINGINE YOTE MIKUBWA"

Post a Comment