Ikiwa kitu unachotaka kufanya ni sahihi, na unakiamini,
endelea kufanya! Iweke ndoto yako mbele, na kamwe usijali kile “wanachokisema” ikiwa
utakutana na anguko la muda, kwa kuwa labda, hawafahamu kwamba, kila
anguko huja likiwa limebeba mbegu ya mafanikio yenye ukubwa sawa na anguko
lenyewe.
Henry Ford, aliyekuwa masikini na ambaye hakuwa na elimu,
aliota juu ya gari lisilokokotwa kwa farasi. Alikwenda kufanya kazi akitumia
zana alizokuwa nazo pasipo kusubiri fursa nzuri imjie, na sasa ushahidi wa
ndoto yake umetapakaa duniani kote. Ameyafanya matairi mengi zaidi kuzunguka
kushinda mtu mwingine yeyote yule aliyewahi kuishi kwasababu hakuwa mwoga
kuzisukuma mbele ndoto zake.
Thomas Edison aliota ndoto ya taa ambayo ingeweza kuwaka
kwa kutumia umeme. Licha ya kufeli mara elfu kumi, aliisimamia ndoto yake hiyo
mpaka ilipogeuka kuwa kitu halisi. Waotaji ndoto kivitendo huwa hawakati
tamaa!
Lincoln aliota ndoto ya Uhuru kwa watumwa weusi, akaiweka
ndoto yake katika vitendo, na kwa bahati mbaya alifariki kabla ya kuiona
Kaskazini na Kusini zikiungana
zikiitafsiri ndoto yake kuwa kweli.
Wright Brothers(waliokuwa ndugu wawili) waliota ndoto ya
mashine yenye uwezo wa kuruka kupitia angani. Sasa mtu anaweza kuona ushahidi duniani kote kwamba
walichokiota kilikuwa sahihi. Marcon aliota ndoto ya mfumo kwa ajili ya
kuzitumia nguvu zisizoshikika zilizopo juu angani. Ushahidi kwamba hakuota
ndoto bure, unaweza ukaonekana katika kila redio, TV na simu za mkononi
duniani.
Si hivyo tu ndoto ya Marcon ilizileta nyumba za hali ya
chini kabisa kuwa kandokando ya majumba
makubwa ya kifahari. Ilifanya watu wa kila Taifa juu ya Dunia kuwa jirani kwa
kutengeneza njia ya mawasiliano ambapo habari, taarifa na burudani ziweze
kusambazwa mara moja dunia nzima
Inaweza kukuvutia kujua kwamba “marafiki” wa Marcon
walimchukua na kumweka kizuizini, na kumchunguza katika hospitali ya magonjwa
ya akili wakati Marcon alipotangaza kwamba alikuwa amegundua kanuni ambayo
angeweza kuitumia kutuma ujumbe kupitia hewani pasipo kutumia waya wala njia
nyingineyo inayoweza kushikika ya mawasiliano.
Waotaji ndoto wa leo wanatendewa vyema. Dunia si ngeni
tena kwa ugunduzi mpya. Kwa kweli imeonyesha utayari wa kuwalipa waotajindoto
ambao huipa Dunia wazo jipya. Dunia imejazwa fursa tele ambazo
waotajindoto wa zamani kamwe hawakuzijua. Shauku kubwa ya kuwa na kutenda ni
alama ya kuanzia ambayo muotajindoto ni lazima aanzie.
Ndoto hazizaliwi hivihivi tu kivivu pasipokuwa na
malengo. Dunia haiwakejeli tena waotajindoto, wala kuwaita ni wenye maneno
matupu yasiyotekelezeka. Kumbuka pia kwamba wale wote wanaofanikiwa katika
maisha, huanzia na mwanzo mbaya, na kupitia mapambano mengi yenye kuumiza moyo
kabla “hawajafika”.
Kipindi muhimu
katika maisha ya wale wanaofanikiwa kwa kawaida huja katika kipindi cha
matatizo, ambapo kupitia kwayo hujitatambulisha “nafsi zao za pili”. John
Bunyan aliandika “The Pilgrim’s Progress”(Maendeleo ya Mahujaji) baada ya kuwa
amefungiwa gerezani na kupewa adhabu kali kutokana na mtazamo wake wa kidini.
O. Henry alikigundua kipaji kilichokuwa kimelala ndani ya
ubongo wake baada ya kukutana na mkosi mkubwa, na alifungiwa ndani ya chumba
cha gereza huko Columbus, Ohio. Kwa kusukumwa na hali ngumu aliyokuwa akiipitia
kutambua “nafsi yake ya pili” na kwa kutumia ubunifu wake, aligundua
mwenyewe kwamba alikuwa mwandishi mkubwa badala ya mhalifu mwenye mateso na
aliyetengwa na jamii.
Njia za maisha zipo za aina nyingi na za ajabu na bado uwezo
usiokuwa na kikomo ni wa ajabu ambapo kupitia huo watu wakati mwingine
hulazimika kupitia kila aina ya adhabu kabla ya kugundua akili zao na uwezo wao
wenyewe wa kuzalisha mawazo yenye manufaa kupitia ubunifu.
Itaendelea sehemu ya tano (v)..............................
Itaendelea sehemu ya tano (v)..............................
0 Response to "WAOTA NDOTO KIVITENDO HUWA HAWAKATI TAMAA"
Post a Comment