NJIA ZA KUINGIZA KIPATO CHA ZIADA NJE YA KAZI YAKO | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NJIA ZA KUINGIZA KIPATO CHA ZIADA NJE YA KAZI YAKO

Kuna wakati niliwahi kuandika makala isemayo, HAKUNA UTAJIRI WA MIUJIZA KWENYE MITANDAO:FANYA KAZI”, makala hiyo, sikuwa na maana kuwa haiwezekani mtu akatengeneza pesa kupitia mtandao wa intaneti au katika blogu na tovuti, bali maana yangu ilikuwa kwamba. “unaweza ukapata utajiri wa pesa au mali kwa njia ya kupitia mtandao wa intaneti, lakini siyo kimiujiza kama watu wengi walivyokuwa wakifikiria hapo kabla.

Miaka tuseme kama mitatu mpaka mitano iliyopita, dhana hii ya kujiingizia kipato kupitia mtandao wa intaneti ilikuwa bado ni changa sana hapa Tanzania, na kwa kweli watu wengi walikuwa na fikra nyingi hasi ama zisizokuwa sahihi juu ya utajiri wa kwenye mitandao, tovuti na blogu. Nayasema haya siyo kwa kubuni bali ni kwa ushahidi niliokuwa nao tena ambao nilishuhudia mwenyewe binafsi baada ya kufanya utafiti wa kina.

Mwaka 2011 nilimaliza kutunga kitabu changu ambacho siogopi kusema kilikuwa ni kitabu kilicholeta mapinduzi makubwa mno katika tasnia nzima ya elimu ya pesa na mafanikio nchini kupitia mitandao na hata kupitia sekta nyinginezo za kiuchumi. Kitabu cha MIFEREJI YA PESA NA SIRI MATAJIRIWASIYOPENDA KUITOAkilikuwa ni kitabu cha maajabu” (magic book) kwani kila aliyebahatika kukisoma kitabu kile, alipata mwamko wa ajabu kuhusiana na maisha na kutafuta pesa kwa ujumla.

NI ATHARI GANI MIFEREJI YA PESA ILIACHA AKILINI MWA WALE WALIOKISOMA?
Kuchapishwa kwa kitabu Mifereji ya Pesa kuliambatana na miradi mingine mitatu ambayo ilikuwa ni Tovuti(website) iliyojulikana kama “KUELEKEAUTAJIRI”, blogu ambayo nayo tuliipa jina hilohilo pamoja na kitabu kingine kikubwa tulichokibatiza jina hilohilo. Mara tu baada ya vitu hivyo kukamilika na matangazo kuanza tulishuhudia misururu ya simu za watu, barua-pepe pamoja na ujumbe mfupi wa maneno, wakitaka kujua zaidi kuhusiana na kampuni yetu.

Athari zilikuwa ni za aina mbili, chanya na hasi, kwa upande wa athari chanya, watu wengi waliokisoma kitabu hiki walihamasika sana, vijana wengi wakaanzisha blogs mbalimbali kwa ajili ya kujiingizia pesa, makampuni pamoja na kujitambua upya kwamba wanapaswa kuwa na malengo fulani katika maisha ndipo waweze kufanikiwa kiuchumi, kimasomo au katika nyanja nyingine yeyote ile.

Niligundua dhamira yetu kuu ya kuona wafanyibiashara wadogo wengi kadiri iwezekanavyo wanapiga hatua kuelekea mafanikio, ilikuwa ikifanikiwa na kufanya kazi  baada ya kuona 'bloggers'(wanablogu) wengi wapya wakianzisha blogu na hata wengine wakikopi makala kutoka katika tovuti na blogu yetu.

Kwa kifupi ni kwamba mtu unapokisoma kitabu hicho kinaamsha ndani yako hamu kubwa ya kumiliki biashara yako mwenyewe, hamu ya kuanzisha blogu au tovuti ya kutengeneza pesa, hamu ya kutajirika kupitia mtandao wa intaneti, shauku kubwa ya kuanzisha kampuni yako hata kama huna maelfu ya shilingi, hamu ya ku tengeneza fedha kupitia blogu au tovuti yako, kujua mbinu mbalimbali za kutengeneza pesa ukiwa nyumbani.  nk. 

Kitabu cha “Mifereji ya Pesa na siri matajiri wasiyopenda kuitoa”
Athari nyingine chanya ilikuwa ni; kuongezeka kwa mwamko wa watu mbalimbali waliofanikiwa kimaisha hususani kiuchumi, kuweka wazi siri zao mbalimbali walizopitia katika kufanikiwa. Kama wewe ni mdadisi, hebu jaribu kufanya kautafiti hata kasikokuwa rasmi tu, tangu mwaka 2011 kuona ni kiasi gani matajiri na watu mbalimbali waliofanikiwa kiuchumi  walivyoweka wazi njia mbalimbali za jinsi mtu anavyoweza akaondokana na umasikini kwa kupitia njia mbalimbali halali, kitu ambacho hapo kabla ya hiyo kampeni yetu kuanza kilikuwa siyo kitu cha kawaida watu kuweka wazi siri zao za utajiri au siri za mafanikio.

Mwamko mkubwa zaidi wa watu kutaka kufahamu ni nani mtu tajiri zaidi Tanzania au watu matajiri zaidi Afrika Mashariki, mtu tajiri kuliko wote Duniani, Tajiri mwenye umri mdogo kuliko wote, Mwanamke tajiri kushinda wote  Afrika na Dunia kwa ujumla.nk. 

Kulikuwa na athari hasi kitabu cha mifereji ya pesa kilichoacha kwa wasomaji wetu na miongoni mwazo ni hii ya watu kudhani ya kwamba kampuni yetu pamoja na kampeni tuliyokuwa tukiiendesha iliyoitwa “Kuelekeautajiri” ilikuwa na malengo ya kuwasajili au kuwavutia watu ili wajiunge na taasisi za siri zinazohusika na kuwatajirisha watu kimiujiza, na hili lilitokana na jina letu kuwa na “ukakasi”. Hali hii ilitulazimu kufanya marekebisho makubwa “rebranding” ya majina ya vitabu pamoja na mitandao yetu yaani blogu, ‘website’, na mitandao ya kijamii kama makala hii ya, “hakuna utajiri wa miujiza kwenye mitandao, fanya kazi kwa bidii”, inavyoeleza.

Tukio lililonishtua ni siku moja, aliponipigia simu mtu mmoja aliyejitambulisha ni mkazi wa Kinondoni na yakuwa baada ya kutusoma kwenye tovuti yetu na blogu, alikuwa na shauku ya kuonana na sisi kwani alikuwa na mipango ya kuanzisha mradi wa kutengeneza filamu inayohusiana na maswala ya utajiri. Mwanzoni nilitaka ‘kumpotezea’ na kumjulisha kuwa sisi tunashughulika na vitabu tu na wala hatufadhili miradi ya aina yeyote ile, lakini alinishawishi sana nikutane naye hata ikibidi tuingie ubia kutokana na yeye kuwa tayari anao wafadhili wa uhakika wa kutoa fedha za mradi.

Nilimkubalia tukapanga kukutana Rozana stendi ya mabasi katika mkahawa mmoja jirani. Katika mazungumzo yetu nilibaini hakuwa na lolote kuhusiana na filamu bali lengo lake lilikuwa ni kunihoji ikiwa kampuni yetu ilikuwa na uhusiano na vyama tata vinavyohusishwa na maswala ya utajiri wa miujiza. Niligundua japo hakupenda kunijulisha kuwa alikuwa mwandishi wa habari kutoka chombo fulani cha habari tena kinachoheshimika na bila shaka alikuwa amepewa “assignment” na mkuu wake wa kazi. Akiwa amekificha kinasa sauti chake nisikione, alijaribu kuelekeza mazungumzo yetu kwenye mada zinazohusiana na vyama hivyo akitaka ahakikishe ikiwa kweli tulikuwa tunahusiana nao ama la.

Tuliongea kirafiki sana nikamuelezea kwa ufasaha malengo ya kampuni yetu, na kile tulichokuwa tumekusudia kuwaelimisha watu hususani wafanyabiashara wadogo wanaoanzisha biashara zao pasipokuwa na elimu ya ujasiriamali ya kutosha. Kwa kweli baada ya ‘interview’ hiyo, siku ileile nilichukuauamuzi wa kwenda kubadilisha kabisa muonekano mzima wa blogu, tovuti na vitabu vyetu ikiwa ni pamoja na kubadilisha kabisa jina lililokuwa likiwapa watu tashwishi.

Vile vile ilitubidi kufanya kazi ya ziada kuandaa makala mbalimbali kama hii hapa zilizotoa elimu na ujumbe kuwa mitandaoya kijamii na mtandao wa Intaneti kwa ujumla haikulengwa kwa ajili ya shughuliza kuleta uharibifu kwa wanadamu au hata kuwasaidia “wajanjawajanja” wanaopenda kula pasipo hata kutoa jasho kidogo au kutumia akili zao katika vitu vyenye mitazamo chanya na hivyo kwa mtu yeyote eti kuanza kusaka mitandaoni njia za kimiujiza za kutajirika haikuwa sahihi bali upotofu ulioenezwa na wajanja wachache kwa sababu zao binafsi.

Matokeo ya kubadilisha majina ya mitandao yetu ghafla kwenye google na “search enginse” nyingine yalikuwa na athari mbaya sana kwa idadi ya watu waliokuwa wakitutembelea kwani, idadi ilishuka ghafla kutoka watu 200-300 kwa siku mpaka kufikia  watu 20-50 kwa siku. Tukajifunza somo kubwa sana kuhusiana na hii mitandao kumbe unapobadilisha vitu kama majina, anuani(url) basi kama usipokuwa makini ukatumia kanuni zinazotakiwa utajutia kubadilisha.

Njia za kuingiza pesa(kipato cha ziada) nje ya kazi zako za kawaida.
Uchawi wa kitabu hiki, kama nilivyotangulia kusema kwamba ni kitabu cha maajabu au ‘magic book’, upo katika eneo hili, namna ya kujitengenezea ukwasi wa ziada na huku ukiendelea na ratiba zako za kawaida, iwe ni kazi, masomo au hata biashara yako ya msingi uliyoizoea. 
Mwanamke mjasiriamali akitengeneza pesa kupitia mtandao/blogu yake.
Pamoja na njia nyinginezo 6 za ukweli za kujiingizia pesa hata ukiwa umelala, au ukiwa umelazwa hospitalini pengine kwa bahati mbaya umeugua, au ukiwa umesafiri kwenda kuwajulia hali ndugu na jamaa zako waliokuwa mbali, kuna hii njia yenye nguvu sana ya kujitiririshia noti kirahisi kabisa kupitia mtandao wa intaneti, tovuti au blogu yako unayoweza kuanza biashara hata na mtaji wa shilingi elfu kumi 10,000/= pekee.


0 Response to "NJIA ZA KUINGIZA KIPATO CHA ZIADA NJE YA KAZI YAKO"

Post a Comment