NAOMBA NYIMBO ZA JOSE CHAMELEONE: TUBONGE NA VALU VALU | JIFUNZE UJASIRIAMALI

NAOMBA NYIMBO ZA JOSE CHAMELEONE: TUBONGE NA VALU VALU

Nimepokea simu na barua pepe za wasomaji wetu wengi wakitaka tuweke historia za watu mashuhuri hasa matajiri, wanamuziki, wacheza filamu, wacheza soka na wengineo, lakini tujikite zaidi katika utajiri waliokuwa nao na jinsi walivyoweza kufanikiwa, ni mbinu zipi walizozitumia mpaka wakapata mafanikio hayo.

Bila shaka kila mtu anayefanikiwa maisha ni lazima awe mjasiriamali, kwa hiyo basi katika makala tutakazokuwa tukizijadili kuhusiana na mada hiyo kwenye blogu hii tutajaribu kuwachambua watu hao maarufu kusudi tuweze kubaini ni tabia gani, au sifa zipi za kijasiriamali zilizoweza kuwafikisha pale walipo. Kumbuka tabia/sifa za kijasiriamali zipo nyingi lakini inategemea ni ipi na katika mazingira gani mtu ameitumia.

Miongoni mwa wasomaji waliotuma ushauri ni pamoja na Mbaruk wa Bukoba, yeye ameshauri ikiwezekana tuwe tunasimulia jinsi watu mbalimbali mashuhuri na matajiri walivyoweza kufikia pale walipo na sababu zilizowanyanyua. Anselm Sabas wa Moshi yeye aliomba nyimbo mbili za mwanamuziki mashuhuri Afrika Mashariki Jose Chameleon, Tubonge na Valuvalu, tafsiri ya mashairi yake, utajiri aliokuwa nao pamoja na historia yake kimaisha kwa ujumla.


Tunathamini  mno maoni na ushauri wa wasomaji wetu, hivyo kuanzia leo tutaanza kutekeleza kile mlichoomba bila ya hiyana na kwa kuanza basi tumeonelea tuanze na huyu Gwiji Jose Chameleon kutoka nchini Uganda na kabla ya yote kwanza hebu tuzisikilize ngoma zake mbili pamoja na video zilizoombwa na msomaji wetu kutoka moshi Anselm Sabas.


Tubonge wimbo uliompa chameleone umaarufu mkubwa.

Video ya wimbo huo Tubonge(official video)


Sasa unaweza kudownload mp3 ya  wimbo  wa Valu valu hapa.



                    VIDEO ya wimbo Valu valu,tazama hapa chini.

0 Response to "NAOMBA NYIMBO ZA JOSE CHAMELEONE: TUBONGE NA VALU VALU"

Post a Comment