MUIGIZAJI ALIYEACHA DAWA ZA KUREFUSHA MAISHA ARVS AFARIKI DUNIA | JIFUNZE UJASIRIAMALI

MUIGIZAJI ALIYEACHA DAWA ZA KUREFUSHA MAISHA ARVS AFARIKI DUNIA

Lesego Motsepe enzi za uhai wake
Aliyekuwa muigizaji  mashuhuri wa Tamthiliya ya “Isidingo The Need” “Lesego Motsepe” miaka 39 amefariki dunia baada ya kupambana na Virusi vya Ukimwi kwa takribani muda wa miaka 15.

Akijulikana kwa jina la Ustaa la ‘Letti Matabane’ tangu mwaka 1998 hadi mwaka 2008 ‘Lesego’ alifanya kazi ya uigizaji, sambamba na kutoa ‘speech’ za kuwatia watu moyo na kuhamasisha, “motivational speeches” vilevile alikuwa ni balozi wa Ukimwi.

Alijitangaza rasmi kuishi na virusi vya ukimwi  siku ya ukimwi Duniani hapo Desemba 1  2011 na kusema kuwa  alikuwa akiishi na hali hiyo tokea mwaka 1998.

Aliacha matumizi ya dawa za kurefusha maisha ‘ARVS’ kinyume na ushauri wa daktari wake hapo July 2012 kwa madai kwamba alikuwa anataka kuhamia kutumia dozi  takatifu “Holistic regimen” yaani tiba kwa njia ya tafakuri au “Meditation”, matumizi ya mitishamba, “Beetroot diet” pamoja na kula vitunguu swaumu.



Alisema kwamba asingeweza kuendelea na wazo la kutumia ‘ARVS’ katika muda wa maisha yake wote uliokuwa umesalia.

0 Response to "MUIGIZAJI ALIYEACHA DAWA ZA KUREFUSHA MAISHA ARVS AFARIKI DUNIA"

Post a Comment